.
JIKONI FESTIVAL TANZANIA ni jukwaa la kitaifa linalotumia chakula kama kiunganishi cha uzalishaji, viwanda, masoko, uwekezaji, utalii, utamaduni, mazingira na uwezeshaji wa kiuchumi.
Tofauti na tamasha la chakula linalolenga maonesho na burudani pekee, JIKONI imeundwa kuwa jukwaa la soko na ukuaji wa biashara, likichanganya maonesho na mauzo, usindikaji na viwanda vidogo, pamoja na kuwezesha mahusiano ya B2B.
Dira: Kuwa jukwaa kuu la Kitaifa linalounganisha chakula, biashara, uwekezaji, utamaduni na maendeleo ya jamii.
Lengo Kuu: Kukuza mnyororo wa thamani wa chakula na vinywaji Tanzania kupitia ukuaji wa masoko, Viwanda, uwekezaji, uwezeshaji wa wajasiriamali na Utalii wa Chakula.
Maonyesho & Biashara
Wahusika: Mama Lishe na Baba Lishe.
Pilau, biryani, wali, ugali, ndizi, chipsi, vitafunwa, street food na vyakula vya asili.
Wahusika: Wachoma Nyama / Wamiliki wa Majiko.
Nyama choma, BBQ, kuku, mbuzi, ng'ombe, samaki, dagaa, kamba na vyakula vya baharini.
Wahusika: Kampuni, viwanda na wadau.
Kahawa, chai, cocoa/chocolate beverages, juices za asili na vinywaji vya mimea.
Wahusika: Wakulima wa zabibu, Viwanda na Wauzaji.
Wachakataji, Viwanda vya Mvinyo, Chapa za mvinyo na wadau wa mnyororo wa thamani.
Wahusika: Wakulima, Wauzaji na Wasambazaji.
Viungo, asali, bidhaa za nyuki, herbs, sauces, seasonings na natural food products.
Wahusika: Wakulima na Wasambazaji.
Organic foods